Tiketi na Bei ya Viingilio vya Wiki ya Mwananchi 2025

Tiketi na Bei ya Viingilio vya Wiki ya Mwananchi 2025

Tiketi na Bei ya Viingilio vya Wiki ya Mwananchi 2025 – Timu ya Yanga imeanza kuuza tiketi za tamasha la kilele cha Wiki ya Mwananchi 2025, litakalofanyika tarehe 12 September 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa. Hii ni fursa muhimu kwa mashabiki wa Yanga kujumuika pamoja na kusherehekea klabu yao. Tiketi zimeanza kuuzwa katika Makao Makuu ya Klabu Jangwani, maduka ya TTCL nchi nzima, na kupitia mitandao ya simu.

Ikiwa ni maandalizi ya kuelekea msimu mpya wa 2025/2026 klabu ya Yanga tayari imesha weka hadharani viingilio vitakavyo tumika kwenye sherehe za wiki ya Mwanachini

Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram klabu ya yanga imesha weka gharama za viingilio kwa wiki ya mwananchi itakayofanyika siku ya tarehe 12/09/2025.

Tiketi na Bei ya Viingilio vya Wiki ya Mwananchi 2025

Viwango vya Tiketi:

Hapa chini ni mwongozo wa bei za tiketi za sherehe ya Wiki ya Mwananchi

Mzunguko – Tsh 5,000

Orange – Tsh 10,000

Vip C – Tsh 15,000

Vip B – Tsh 30,000

Vip A – Tsh 50,000

Royal – Tsh 300,000

VVIP – Tsh 600,000

Jinsi ya Kununua tiketi za Wiki ya mwananchi kupitia mitandao ya Simu

Maeneo ya Kununua Tiketi:

  1. Makao Makuu ya Klabu Jangwani: Tiketi zinapatikana kwa urahisi kwa mashabiki wanaoishi karibu na makao makuu ya klabu.
  2. Maduka ya TTCL Nchi Nzima: Mashabiki wanaweza kupata tiketi kwenye maduka ya TTCL yaliyoenea kote nchini.
  3. Mitandao ya Simu: Kwa urahisi zaidi, tiketi zinaweza kununuliwa kupitia huduma za mitandao ya simu, kurahisisha upatikanaji wake bila kwenda moja kwa moja kwenye vituo vya mauzo.

Mashabiki wote wa Yanga wanahimizwa kuchukua tiketi mapema ili kuepuka usumbufu na kuhakikisha wanapata nafasi ya kushiriki katika tamasha hili kubwa la Wiki ya Mwananchi 2025.

error: Content is protected !!