TAMISEMI: FORM FIVE SELECTION 2025/2026

_________________________________________________

MATANGAZO YA AJIRA  KILA SIKU BOFYA HAPA

_________________________________________________

NOTES ZA KIDATO CHA 1 HADI 6 BOFYA HAPA

_________________________________________________

MAGROUP MAPYA YA WHATSAAP BOFYA HAPA

_________________________________________________
MATANGO YA AJIRA BOFYA HAPA
JIUNGE NASI TELEGRAM BOFYA HAPA

Vigezo na Sifa za Kujiunga JKT Mujibu Wa Sheria

Filed in Makala by on September 17, 2024 0 Comments

Vigezo & Sifa za Kujiunga JKT Mujibu Wa Sheria

Tangazo

Habari hii na nyingine nyingi zinapatikana kwenye telegram channel yetu na WhatsApp channel yetu tumia linki hapo chini kujiunga

Jeshi la kujenga Taifa(JKT) limekuwa linapokea na kuendesha Mafunzo yahusuyo Ulinzi wa Taifa, uzalendo, Ujasiliamali, Ujasili (kupitia mafunzo ya Kilimo, Ufugaji na Biashara) kwa nyakati tofauti tofauti kadri ya maelekezo kutoka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Vijana wa JKT wamegawanyika katika makundi mawili nayo ni

  1. Vijana wa Kujitolea na
  2. Vijana wa Mujibu wa Sheria

Vijana wa Kujitolea

Hawa ni vijana wa JKT ambao wanajiunga na JKT kwa Mkataba wa kujitolea kwa kipindi kisichopungua miaka miwili (2). Mara baada ya kuandikishwa vijana hao huwa wanapelekwa kwenye kambi mbalimbali za JKT kwa ajili ya Malezi na Mafunzo mbalimbali.

Vijana wa Mujibu wa Sheria

Hawa ni wale vijana wanaojiunga na JKT kwa mujibu wa sheria. Kwa mujibu wa katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, wanatumikia JKT kwa kipindi kisichopungua miezi (3). kwa sasa vijana wa Mujibu wa sheria ni wale wanafunzi waliomaliza kidato cha sita (form six) kutoka mashule mbalimbali ya Tanzania Bara.

Masharti ya kijana wa kujitolea kwa ajili ya kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa

1. Awe raia wa Tanzania

2. Awe na Umri kati ya miaka 18-23

3. Awe amemaliza darasa la saba na kuendelea

4. Asiwe ameoa au kuolewa na asiwe na mtu yeyote anayemtegemea

5. Awe tayari kufuata sheria zote za kijeshi zitazokuwa juu yake wakati akiwa jeshini(kutoroka,wizi,ulevi,uvutaji bangi, madawa ya kulevya na upatikanaji wa mimba n.k) Jeshini ni makosa makubwa na utaweza kushtakiwa na kufutiwa mkataba na JKT

6. Awe tayari kurudi nyumbani baada ya kumaliza mkataba wake na Jeshi la Kujenga Taifa

7. Awe na tabia na mwenendo mzuri

Masharti ya kijana wa mujibu wa sheria kwa ajili ya kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa

1. Awe raia wa Tanzania

2. Awe na Umri kati ya miaka 18-35

3. Awe amemaliza kidato cha sita na kuendelea

4. Awe tayari kufuata sheria zote za kijeshi zitazokuwa juu yake wakati akiwa jeshini(Uvutaji bang, madawa ya kulevya na upatikanaji wa mimba atashitakiwa na kufutiwa mkataba na JKT

5. Utoro haukubaliki na kosa la utoro mkataba utasogezwa mbele

6. Awe na tabia na mwenendo mzuri

UJUE UTARATIBU WA KUJIUNGA NA JKT

JKT huandikisha vijana wa kujitolea kutoka mikoa yote ya hapa nchini kila mwaka. Utaratibu unaotumika ni kwa JKT kuandika barua kwa wakuu wa Mikoa na kuanisha nafasi ambazo mkoa umetengewa.

Baada ya Mkoa kupata barua kutoka kwa Mkuu wa JKT na idadi ya nafasi za vijana waliopangiwa kujiunga. Mkoa hugawa nafasi hizo kulingana na wilaya zake. Pia wilaya zinatakiwa kupeleka katika tarafa, kata na vijiji. Mara nyingi uongozi wa wilaya hubandika tangazo la nafasi hizo katika ubao wao wa matangazo. JKT hutangaza nafasi za kujiunga na jeshi hilo kupitia vyombo vya habari vya Serikali na biafsi kwa nia ya kuharakisha taarifa kuwa. kia wananchi hasa vijana. Usaili wa awali hufanyika chini ya Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya wanakotoka vijana hao, baadaye hufanyika mkoani, ili kupata idadi ya vijana wa mkoa mzima.

Zoezi hilo linapokamilika mikoani, JKT hutuma timu za maafisa na askari kutoka Makao Makuu ya JKT kwa ajili ya kuhakiki vijana waliosailiwa katika mikoa yote ya Tanzania Bara. Vijana hupimwa afya zao na kusafirishwa katika vikosi vya JKT

Mapendekezo ya Mhariri;

1. Ratiba ya Mechi Za Leo Ligi Mbali Mbali Duniani

2. Ratiba Ya Ligi Kuu England 2024/2025 EPL

3. Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025

4. JINSI ya Kupata TIN Number Online

5. Jinsi Ya Kuangalia usajili wa kampuni BRELA

6. Orodha ya Kambi za JKT Tanzania

Asante kwa kusoma makala yetu hadi mwisho, ikiwa una maswali yoyote tafadhali acha maoni hapa chini au unaweza Wasiliana nasi. Usisahau kujiunga nasi kwenye WhatsApp gropu letu kwa updates zaidi.

Jiunge na Whatsap Gropu letu kwa updates za kila siku

BONYEZA HAPA

MATANGO YA AJIRA BOFYA HAPA
JIUNGE NASI TELEGRAM BOFYA HAPA

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *