Ratiba ya Mechi za Yanga Klabu Bingwa Afrika 2024/2025, Habarin mpezi wa soka wa Habarika24, katika makal hii ya michezo tutaenda kutazama ratiba ya mechi za klabu ya yanga kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika msimu wa 2024/2025 (CAF Champions League). Kama wewe ni shabiki wa michuano ya klabu bingwa Afrika basi ni muhimu kutazama ratiba kamili ya michuano hii na pia kama ni mpenzi na shabiki wa klabu ya Yanga basi hapa tunakuwekea ratiba kamili ya mechi zote za Yanga kwneye hatua za makundi.
Shirikisho la soka barani Afrika limesha chezesha droo ya ,amakundi na kutangaza makundi ma nne ambayo yatakua na timu nne kwenye kila kundi katika hatua hii ya makundi. Huku tukishuhudia makundi ya vifo kama vile kundi la Yanga kundi A.
Ratiba ya Mechi za Yanga Klabu Bingwa Afrika 2024/2025
Timu zinazoshiriki Katika Hatua ya Makundi Klabu Bingwa Afrika
Kunajumla ya timu 16 ambazo zimefuzu hatua ya makundi na ndio zitakazo shiriki hatua hii ya makundi katika michuano ya klabu bingwa barani Afrika kwa msimu huu wa 2024/2025 kutoka mataifa mbali mbali ya Afrika. Huku Taifa la Tanzania likishuhudia klabu yake ya Yanga Ikitinga katika hatua hiyo ya makundi na ikipangwa katika kundi A
Timu Zilizoko katika Kundi la Yanga Kundi A
Kundi A limetafsiriwa kuwa kundi la kifo kwa kuwa na timu zenye uwezo wa hari ya juu kama yanga nyenyewe na nyinginezo. Hapa tutakuonyesha Timu zinazo unda kundi A.
- TP Mazembe (DR Congo)
- Yanga (Tanzania)
- Al Hilal SC (Sudan)
- MC Alger (Algeria)
Hapo juu ndio timu zinazo unda kundi A, Ili kutanzama makundi mengine ya michuano ya Klabu Bingwa Barani Afrika tafadhari unaweza kubonyeza HAPA

Ratiba ya Mechi za Yanga Klabu Bingwa Afrika 2024/2025
Hii hapa chini ndio ratiba kamili ya michezo yote ya klabu ya YANGA katika michuano ya klabu bingwa Afrika katika hatua ya makundi
Raundi ya Kwanza (Round 1) – 26.11.2024 (14:00)
- Young Africans (Tan) vs Al-Hilal Omdurman (Sud)
Raundi ya Pili (Round 2) – 06.12.2024 (14:00)
- MC Alger (Alg) vs Young Africans (Tan)
Raundi ya Tatu (Round 3) – 13.12.2024 (14:00)
- TP Mazembe (Drc) vs Young Africans (Tan)
Raundi ya Nne (Round 4) 03.01.2025 (14:00)
- Young Africans (Tan) vs Mazembe (Drc)
Raundi ya Tano (Round 5) 10.01.2024 (14:00)
- Al-Hilal Omdurman (Sud) vs Young Africans (Tan)
Raundi ya Sita (Round 6) 17.01.2025 (14:00)
- Young Africans (Tan) vs MC Alger (Alg)
Katika hatua hii ya makundi klabu ya Yanga inatarajia kucheza michezo isiyopungua 6 huku michezo mitatu ikicheza ugenini na michezo mingine 3 ikicheza uwanja wake wa nyumbani. Hivyo kukamilisha michezo yake sita.
Changamoto na Matumaini
Yanga inakabiliwa na changamoto kadhaa:
- Ratiba yenye msongamano wa mechi za ndani na nje
- Kusafiri umbali mrefu kwa mechi za ugenini
- Hali ya hewa tofauti katika nchi mbalimbali
Hata hivyo, kuna sababu kadhaa za kuwa na matumaini:
- Wana wachezaji wa kimataifa wenye uzoefu
- Kocha mpya mwenye ujuzi wa michuano ya Afrika
- Msaada mkubwa kutoka kwa mashabiki
Maandalizi ya Timu
Yanga SC imekuwa ikifanya mazoezi makali kwa ajili ya michuano hii. Wachezaji wamekuwa wakipata mafunzo maalum na timu ya utabibu imehakikisha kwamba wote wako katika hali nzuri ya kimwili.
Msaada wa Mashabiki
Mashabiki wa Yanga, walio wengi wakiitwa ‘Wananchi’, wamekuwa wakionyesha msaada mkubwa kwa timu yao. Kila mechi ya nyumbani inatarajiwa kujaa uwanja, huku mashabiki wakiimba na kuwatia moyo wachezaji wao.
Hitimisho
Ratiba ya Yanga SC katika Michuano ya Klabu Bingwa Afrika inaonyesha safari ndefu na yenye changamoto mbele yao. Hata hivyo, kwa msaada wa mashabiki wao waaminifu na maandalizi mazuri, Yanga ina nafasi nzuri ya kufanya vizuri katika michuano hii. Mashabiki wote wa mpira wa miguu Tanzania wanasubiri kwa hamu kuona jinsi ‘Wananchi’ watakavyofanya katika jukwaa hili la Afrika.
Mapendekezo ya Mhariri;
1. Makundi ya Klabu Bingwa Africa Msimu wa 2024/2025
2. Ratiba Ya Mechi za Chelsea Zilizobaki Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) 2024/2025
3. Ratiba Ya Mechi Za Simba SC Zilizobaki Ligi Kuu Ya NBC Msimu Wa 2024/2025
4. Ratiba ya Mechi Za Leo Ligi Mbali Mbali Duniani
5. Mchezaji mwenye Magoli mengi Tanzania
Asante kwa kusoma makala yetu hadi mwisho, ikiwa una maswali yoyote tafadhali acha maoni hapa chini au unaweza Wasiliana nasi. Usisahau kujiunga nasi kwenye WhatsApp gropu letu kwa updates zaidi.
Jiunge na Whatsap Gropu letu kwa updates za kila siku