NAFASI za Kazi Zilizotangazwa Leo UTUMISHI 2025
Sekretarieti ya Ajira ni chombo muhimu cha serikali nchini Tanzania kinachoshughulikia usimamizi wa ajira katika Sekta ya Umma. Chombo hiki kina jukumu la kuweka mfumo thabiti wa kuandaa, kusambaza, kufuatilia, na kudhibiti nafasi za ajira zote za serikalini. Lengo lake kuu ni kuhakikisha kuwa michakato yote ya ajira inaendeshwa kwa ufanisi, uwazi, na haki kwa wote wanaohitaji kutumika katika sekta hiyo muhimu. Sekretarieti hii hufanya kazi kwa kushirikiana kwa karibu na wizara, idara, na mashirika mbalimbali ya serikali ili kuwezesha upatikanaji wa wafanyakazi wenye sifa na uwezo unaohitajika.
Katika utendaji wake wa kila siku, Sekretarieti ya Ajira huwa na wajibu wa kutangaza nafasi wazi za kazi kupitia vyombo rasmi, kukusanya maombi ya watafutaji kazi, na kusimamia michakato ya uteuzi ili kuhakikisha kuwa inafuata kanuni na taratibu zilizowekwa. Pia inachukua jukumu la kuandaa na kusambara taarifa kuhusu fursa za ajira na mabadiliko yanayohusu ajira za umma kwa umma. Kwa kufanya hivyo, Sekretarieti ya Ajira inachangia kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha utawala bora, kupunguza ukiritimba, na kuhakikisha usawa na uadilifu katika usambazaji wa fursa za ajira katika sekta ya umma ya Tanzania, na hivyo kuleta imani ya umma katika mifumo ya ajira ya serikali.
NAFASI za Kazi Zilizotangazwa Leo UTUMISHI
Ili kuweza kusoma aina ya kazi, vigezo na jinsi ya kutuma maombi tafadhari bonyeza kwenye kila tangazo la kazi hapo chini
Naomba kufanya kazi katika kampuni yenu