NAFASI 57 za Kazi Taasisi Mbalimbali za Umma June 2025
Sekretarieti ya Ajira ni chombo muhimu cha serikali kinachoshughulikia masuala ya ajira na uajiri nchini Tanzania. Chombo hiki kimeundwa kwa lengo la kuhakikisha kuwa wananchi wanapata fursa sawa za ajira na kukuza uwezo wao wa kibiashara na kitaaluma. Sekretarieti ya Ajira hufanya kazi kwa kushirikiana na mashirika mbalimbli ya umma na binafsi ili kuweka mfumo wa ajira unaofaa na wa haki. Pia, inaweka mikakati ya kuwapa vijana na watafuta ajira mafunzo na ujuzi wa kutosha ili kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika soko la kazi.
Miongoni mwa malengo ya Sekretarieti ya Ajira ni kukuza utoaji wa huduma bora kwa watafuta ajira na kuhakikisha kuwa fursa za ajira zinapatikana kwa uwazi na haki. Chombo hiki pia hudumisha mfumo wa kielektroniki wa ajira (ajira portal) ambapo wananchi wanaweza kutuma maombi ya kazi na kufuatilia fursa mbalimbli za kazi. Kwa kufanya hivyo, Sekretarieti ya Ajira inasaidia kupunguza ukosefu wa ajira na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa. Kwa ujumla, Sekretarieti ya Ajira ina jukumu muhimu katika kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya ajira nchini Tanzania.
NAFASI 57 za Kazi Taasisi Mbalimbali za Umma June 2025
Kwa niaba ya Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Tabora (TUWASA) na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Iringa (IRUWASA), Wizara ya Maji, Taasisi ya Maji (WI), na Tume ya Kitaifa ya Mpango wa Matumizi ya Ardhi (NLUPC), Taasisi ya Usimamizi wa Fedha (IFM), Taasisi ya Uhasibu Arusha (IAA), Tume ya Madini, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma inawaalika Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi zilizo wazi 57 (hamsini na saba) kama zilivyotajwa hapo chini.