Matokeo ya Usaili wa Mahojiano TRA May 2025
Dar es Salaam, 27 Mei, 2025
Itakumbukwa kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilitangaza nafasi za kazi 1,596 mwanzoni mwa Februari 2025, ambapo ilipokea maombi 135,027, ambayo 113,023 yaliitwa kwenye usaili wa maandishi baada ya kufikia vigezo, na usaili huo ulifanyika tarehe 29 na 30 Machi, 2025.
Waombi waliofaulu katika usaili wa maandishi waliitwa kwenye usaili wa mazungumzo uliofanyika kati ya tarehe 12 hadi 14 Mei, 2025, ambapo waombi 6,325 waliwasailiwa. Kwa njia maalum, Mamlaka ya Mapato Tanzania inamshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa KUIDHINISHA maombi ya Mamlaka ya kuongeza nafasi za kazi 300 zilizopangwa katika Bajeti ya Mwaka 2025/26 kujazwa katika mchakato huu uliokwisha, hivyo kuongeza idadi ya wafanyakazi wataoajiriwa hadi 1,896 badala ya 1,596 awali.
Mamlaka inapenda kuwataarifu wote waliofanya usaili kuwa matokeo yatatolewa kesho, tarehe 28/05/2025, kupitia barua pepe zao zilizotumika kwa ajili ya maombi ya kazi.
Waombi 1,896 waliofaulu na kuitwa kazini wanatakiwa kufika kwenye vituo vyao vilivyowekwa tarehe 02 Juni, 2025 saa 1:00 asubuhi bila kukosa, wakiwa na vyarafa muhimu kama vilivyoelezwa kwenye barua pepe zao.
Soma Pia;
- PDF ya Majiana Walioitwa Kazini Utumishi (Call For Work) Leo
- Bei ya Tecno Camon 30 Series Na Sifa Kamili
- Bei ya Tecno Camon 12 Pamoja na Sifa Kamili
- Bei ya Tecno Camon 15 Pamoja N a Sifa Zake
- Bei ya Tecno Camon 17 Pamoja Na Sifa Kamili
Mamlaka inawashukuru wote walioonyesha nia ya kufanya kazi na Mamlaka ya Mapato Tanzania, na inawatakia kila la heri katika kujenga Taifa. Pia, waombi 4,429 walioshiriki usaili na hawakuitwa kazini, taarifa zao zitahifadhiwa kwenye hifadhidata ya Mamlaka kwa matumizi ya baadaye.
Kwa maelezo zaidi, wasiliana na Mamlaka kwa maelezo yafuatayo;-
Website: www.tra.go.tz
Toll-free numbers:
0800 780078 or 0800750075 or 0800110016
WhatsApp: 0744 23 33 33
Email: [email protected] or [email protected]