NAFASI 10 za Kazi Bariadi District Council August 2025

Kwa AJIRA Mpya Kila Siku (BOFYA HAPA)

_____________________________________

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi amepokea kibali cha ajira mpya katika mwaka wa fedha 2024/2025 chenye Kumb.Na FA.97/228/01/A/2 cha tarehe 21/04/2025 kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na utawala Bora. Hivyo, Watanzania wenye sifa wanakaribishwa kutuma maombi ya nafasi za kazi zilizoanishwa katika Tangazo hili.

NAFASI 10 za Kazi Bariadi District Council August 2025

MASHARTI YA UJUMLA.

i. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri wa kuanzia miaka 18 na usiozidi miaka 45.

ii. Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha kwenye mfumo wa kuombea ajira ulemavu walionao kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira Katika utumishi wa Umma;

iii. Waombaji wote waambatishe malezo binafsi yaliyojitosheleza (Detail Curriculum Vitae) yenye anuani inayotumika, namba za simu zinazopatikana na Anuani ya Barua
pepe (E-mail address) pamoja na majina ya wadhamini (Referres) watatu wa kuaminika;

iv. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detail C.V) yenye anuani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (Referees) watatu wa kuaminika;

v. Maombi yote yaambatane na vyeti vya Elimu na Taaluma vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya Kidato cha Nne au Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. Certificates, – Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI, Computer Certificate, – Vyeti vya Kitaaluma.

vi. “Testimonial”, “Provisional Results”, “Statement of Results”, hati ya matokeo ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.

vii. Waombaji waliosoma nje ya Nchi wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na vimethibitishwa na Mamlaka husika (TCU, NECTA NA NACTE).

viii. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi.

ix. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika utumishi wa Umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika
Waraka Na. CAC.45/257/01/D/140 wa tarehe 30 wa Mwaka 2010.

x. Waombaji kazi wa kada ya Dereva II wenye leseni Daraja E au C wanapaswa KUAMBATISHA vyeti vya mafunzo ya Udereva vilivyowapatia sifa ya kupata madaraja husika

xi. Mwisho wa kupokea maombi itakuwa tarehe 13/08/2025.

BONYEZA HAPA KUTUMA MAOMBI

Share this job

Search Job

Chuo Kikuu cha Mtakatifu John cha Tanzania (St John’s University of Tanzania – SJUT) ni chuo kikuu binafsi kinachomilikiwa na Kanisa la Anglikana Tanzania. Kimeanzishwa kwa lengo la kutoa elimu ya juu yenye msingi wa maadili, maono na huduma kwa jamii. Kiko katika mji wa Dodoma, katikati ya Tanzania, na kinatoa programu mbalimbali kuanzia shahada za kwanza hadi za juu
Smiles Dental Clinic ni kliniki ya kisasa ya meno inayotoa huduma bora kwa wagonjwa wa rika zote. Kliniki hii imejipatia sifa kwa kutumia vifaa vya kisasa na teknolojia ya hali ya juu katika kutibu matatizo mbalimbali ya meno kama vile kung’oa, kusafisha, kuweka dawa, na kufunga braces. Madaktari wake ni wataalamu wenye uzoefu mkubwa katika fani ya afya ya kinywa
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma anapenda kuwataarifu waombaji kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili kati ya tarehe 25-05-2025 na tarehe 05-06-2025 kuwa matokeo ya waombaji kazi waliofaulu usaili huo ni kama yalivyoorodheshwa katika tangazo hili. Orodha ya majina haya pia inajumuisha baadhi ya wasailiwa waliokuwa kwenye kanzidata (Database) kwa kada mbalimbali ambao wamepangiwa vituo vya kazi
Angalia Majina ya Walioitwa Kazini Kupitia UTUMISHI – Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (PSRS) 2025 Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (PSRS) ni chombo cha serikali chenye hadhi ya Idara Huru kilichoanzishwa mahsusi kurahisisha mchakato wa ajira kwa watumishi wa umma. Sekretarieti hii ilianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002
error: Content is protected !!