JINSI ya Kutuma Maombi ya Kazi Tume ya Utumishi wa Mahakama June 2025
BONYEZA HAPA KUPATA FORM YA MAOMBI
JINSI ya Kutuma Maombi ya Kazi Tume ya Utumishi wa Mahakama June 2025, Mfumo wa kutuma maombi ya kazi tume ya utumishi wa Mahakama – Judicial Service Commission – Job Application Portal
Tume ya Utumishi wa Mahakama ni chombo kilichoundwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa lengo la kusimamia masuala ya ajira, nidhamu, na maendeleo ya watumishi wa mahakama. Tume hii ina jukumu la kuhakikisha kuwa mfumo wa utoaji haki unakuwa na watumishi wenye weledi, maadili na ufanisi unaohitajika ili kukuza haki na usawa mbele ya sheria. Pia, hutoa ushauri kwa Mhe. Jaji Mkuu juu ya masuala mbalimbali yanayohusu utumishi wa mahakama ili kuhakikisha kuwa uendeshaji wa shughuli za mahakama unazingatia viwango vya kitaaluma na kisheria.
Majukumu mengine ya Tume ya Utumishi wa Mahakama ni pamoja na kushughulikia masuala ya ajira mpya, kupandisha vyeo, na kushughulikia malalamiko au migogoro ya kiutumishi miongoni mwa watumishi wa mahakama. Kwa kufanya kazi kwa kushirikiana na idara nyingine za serikali na mashirika ya kimataifa, tume hii inasaidia katika kuimarisha mfumo wa haki nchini. Kwa hivyo, Tume ya Utumishi wa Mahakama ni mhimili muhimu katika kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma bora za kimahakama kupitia watumishi waliobobea na wanaowajibika.
Mfumo wa Kutuma Mambi ya Kazi Tume ya Utumishi wa Mahakama
Ili kuweza kutuma maombi ya ajira zilizotangawa na tume ya utumishi wa mahakama tafadhari fuata hatua hizi hapa chini:
Kwanza lazima uwe umesha jisajiri na mfumo wa maombi ya kazi wa tume ya utumishi wa Mahakama,kama bado Bonyeza HAPA kujisajiri sasa
Baada ya kujisajiri fuata hatua hizi hapa
1. Ingia kwenye tovuti rasmi ya Tume ya Utumishi wa Mahakama
2. Kisha bonyeza Sign in kwa kuingiza login detail zako ikiwa ni email address na password ulizotumia wakati wa kufungua account yako.
3. Ukishaingia kwenye mfumo neda sehemu ya HOME na tafuta aina ya kazi unayohitaji kutuma maombi kisha bonyeza neno “Apply”
4. Mfumo utakufungulia form ya kutuma maombi (Judicial Service Commission – Application Form)
5. Form itakutaka ujaze taarifa za msingi.kama vile
A) Taarifa Binafsi(Persoal Details)
- Majina matatu
- Tarehe ya kuzaliwa
- Jinsia na hali ya ndoa
- Mahari unapoishi,Mkoa na namba ya simu
- Kitambusho cha Taifa,Pasport Size na cheti cha kuzaliwa
B) Taarifa za Kitaaluma
- Taarifa za kidato cha nne
- Taarifa za kidato cha sita
- Taarifa za elimu ya juu
C) Taarifa za kuajiriwa
- Kama umeajiwa au hujaajiriwa
Baada ya kujaza taarifa zote kwa usahihi tafadhari pitia tena ili kujiridhisha na taarifa ulizozijaza kama ni za kweli na sahihi
Kisha bonyeza neno ‘Submit Application” hadi hapo utakua umesha fanya application ya ajira.
Tukutakie kila lakheri kwenye safari yako mpya ya matumaini ya ajira za Tume ya Utumishi wa Mahakama