Jinsi Ya Kutoa Pesa Kwenye ATM Ya CRDB Kupitia M-Pesa, kutoa pesa ATM ya CRDB kwa M-Pesa
Habari ya wakati huu mwanahabarika24, karibu katika makala hii fupi itakayoenda kukupa mwongo wa namna ya unavyoweza kutoa pesa kwenye ATM za CRDB kwa kutumia M-Pesa yako.
Kama unahitaji kutoa pesa kupitia ATM ya CRDB na kwa bahati mbaya umesahau cadi yako ya ATM basi usijali kama unamtandao wa simu wa Vodacom uliyosajiliwa na M-Pesa unaweza kuitumia akaunti yako ya M-Pesa kuweza kutoa pesa kwenye ATM ya CRDB kutoka kwenye akaunti yako ya Mpesa.
Kutoa pesa kwenye ATM ya CRDB kwa kutumia M-Pesa ni njia rahisi na salama kuweza kupata fedha zako kutoka kwenye akaunti yako bila kuhitaji kadi ya benki. Kupitia huduma hii, unaweza kutoa pesa yako wakati wowote kutoka kwenye ATM za CRDB kwa kutumia simu yako ya mkononi. Katika mwongozo huu, tutaelezea hatua kwa hatua jinsi ya kufanya muamala huu.
Jinsi Ya Kutoa Pesa Kwenye ATM Ya CRDB Kupitia M-Pesa
Hapa chini tunaenda kukuonyesha hatua zote za kufuata pale unapotaka kutoa pesa kupitia ATM za CRDB kupitia M-pesa yako
Vitu Muhimu vya Kuzingatia Kabla ya Kuanza Mchakato
Hapa chini ni mambo muhimu ya kuzingatia unapotaka kutoa pesa kutoka akaunti yako ya M-Pesa kupitia ATM ya CRDB
- Kuwa na akaunti laini ya Vodacom iliyosajiliwa na M-Pesa
- Akaunti yako ya M-pesa iwe na kiwango cha pesa unachihitaji kutoa
- Kuwa karibu na ATM ya CRDB kwani mchakato huu hufanyika ndani ya dk 5
- Kuwa na simu yako ya mkononi pamoja nawe na iwe na laini hiyo ya vodacom iliyosajiliwa na M-Pesa
- Kuhakikisha una mtandao wa Vodacom
Hatua za Kufuata ili kutoa pesa kutoka ATM ya CRDB kupitia M-pesa
1. Anza Muamala kwenye Simu Yako
Ukiwa kwenye simu yako ndani ya chumba cha ATM ya CRDB fuata hatua zifuatazo
- Fungua simu yako
- Ingia kwenye menyu ya M-Pesa kwa kupiga *150*00#
- Chagua “Toa Pesa”
- Ingiza namaba ya wakala ya CRDB amabyo ni 999999
- Kisha ingiza kiasi unachitaka kutoa
- Ingiza namba ya siri ya M-pesa
- Kisha utapokea ujumbe wenye tarakimu 6 (tarakimu hizi hudumu ndani ya dakika 5 tu)
2. Kwenye ATM ya CRDB
Baada ya kufanya mwamala kutoka kwenye M-Pesa yako kupitia simu yako na kutumiwa msimbo wenye tarakimu 6 sasa fanya hatua zifuatazo kwenye ATM ya CRDB
- Bonyeza kitufe cha M-PESA kinachoonekana kwenye skrini ya ATM ya CRDB
- Kisha ingiza msimbo wa namba ulizotumiwa kwenye simu yako, hakikisha unaingiza tarakimu sahihi
- Weka namba ya simu ya M-Pesa uliyoitumia kutoa pesa
- Chagua kiasi unachotaka kutoa
- Thibitisha kutoa fedha
- Hadi hapo utakua umetoa pesa kutoka akaunti yako ya M-Pesa kupitia ATM ya CRDB
Kwa maelezo zaidi unaweza tembelea tovuti rasmi ya CRBD Bank
Hitimisho
Njia hii inamsaidia mtu mwenye pesa katika akaunti yake ya M-pesa na nahitaji kutoa pesa hiyo lakini mahali alipo hakuna wakala wa M-Pesa anaweza kutumia ATM ya CRDB iliyop[o karibu yake kuweza kutoa pesa zake.
Mapendekezo Ya Mhariri;
1. Jinsi Ya Kukata Tiketi Ya Basi Mtandaoni
2. Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania
3. Jinsi Ya Kulipia King’amuzi Cha Azam Tv
4. Jinsi Ya Kuangalia Salio La NSSF Kwa Njia ya Simu
5. Jinsi Ya Kufanya Biashara Mtandaoni