Fei Toto Rasmi Kutua Simba Sc
Hatimae kiungo mshambuliaji wa klabu ya Azam Fc Feisal Salum Addallah (Fei Toto) inaelezwa kua tayari amelidhia kusajiliwa na Simba Sc baada ya kuwekewa dau kubwa la usajili ikiwa ni pamoja na mshahara kwa mwezi na marupurupu.

Usajiri wa Feisal Salum Simba, Mshahara wake na Marupurupu
Ada ya Usajili; Milioni 800
Mshahara kwa Mwezi; Milioni 50
Pesa za Ziada; Bonasi kwa kila goli na Assist
Baada ya Feisal Salum kukubali kusajiliwa na klabu ya Simba kwa sasa Simba ipo kwenye makubaliano ya mwisho na klabu ya Azam ili kukamilisha zoezi la usajili kwa kiungo mshambuliaji huyo.
Azam kwa upande wao pia wako tayari kumuachia nyota huyo kwenda kujiunga na klabu ya Simba Sc.Pia taarifa za ndani kutoka kwa memeja wa Feisal Salum Addallam ameeleza ya kua hakuna kipengele chochote kinachoeleza kua usajili wa Feisal Salum kwenda Simba klabu ya Yanga itapewa gawio la fedha.