Form Five Notes All Subjects PDF Free Download
Form Five Study Notes All Subjects PDF Free Download, Notes za Kidato cha 5 Masomo yote, Habari mwanakisiwa24, karibu katika page hii itakayoenda kukupa mwongozo wa namna ya kudownload notes za kidato cha Tano kwa masomo yote.
Je, wewe ni mwanafunzi au mzazi wa mwanafunzi aliyeko kidato cha tano na uko mtandanoni kutafuta jinsi ya kuweza kupakua notes za kidato cha tano masomo mbali mbali, basi usijali kwani katika page hii utaweza kupata nafasi ya kudownload form five notes kwa masomo yote bure kabisa.
Jinsi ya Kudownload Form Five Notes Masomo yote
Ili kuweza kupakua notes za kidato cha tano kwa masomo yote tafadhari embu fuata hatua hizi hapa chini;
1. Ukiwa kwenye page hii nenda chini hadi ukute orodha ya masomo ya kidato cha tano
2. Baada ya kuona orodha ya masomo sasa unaweza kubonyeza kwenye somo unalotaka kupakua notes zake
3. Mara baada ya kubonyeza somo ukrasa mwingine utafunguka
4. Ukra huu mpya utakaofunguka utakua wa somo ulilolibonyeza na topic zote za somo hilo
5. Tafadhari fuata maelekezo kama yalivyotolewa kwenye ukrasa wa somo ili kuweza kupakua notes za somo ulilolicagua
Form Five Notes All Subjects PDF Free Download
Hapa chini ni orodha ya masomo yanayofundishwa kidato cha 5, ili kuweza kudownload notes za masomo haya tafadhari bonyeza kwenye somo unalotaka kupakua notes zake kutoka kwenye orodha ya masomo hapo chini
MOFIMU
Mofimu ndio kipashio cha msingi kinachoshughulika katika mofolojia ya lugha kwa maana mbalimbali za mofimu. Baadhi ya wataalamu hujaza mofimu kwa kutumia kigezo cha muundo wa mofimu na wengine hufasili kwa kutumia kigezo cha kazi au dhima zinazobebwa na mofimu husika.
MAANA YA MOFIMU
Mofimu ni sehemu ya neno au neno zima lenye maana ya kisarufi au maana ya kileksika
AU
Mofimu ni kipashio kidogo cha kimofolojia chenye kubeba maana iliyo ya kisarufi au ya kileksika
Mofimu hupangwa kwa kuzingatia utaratibu maalumu ili kujenga maneno yenye maana utaratibu huo hufahamika kama kanuni. Utaratibu wa upangaji wa mofimu ukikiukwa huzalisha maumbo yasiyokubalika katika lugha husika.
Mfano:
a – na – som – a neno hili linakubalika katika lugha kwa sababu mpangilio wake wa mofimu umezingatia kanuni lakini mpangilio wake ungekuwa vinginevyo husingekuwa na maana
Mfano:
som – na – a –a tungezalisha umbo lisilokuwa na maana. Kila lugha inautaratibu wake wa kuzipanga mofimu
N.B Wakati mwingine mofimu huwa na maana sawa na neno, mofimu hizo huitwa mofimu huru au mofimu za kilekisika. Mofimu hizi husimama zenyewe bila kutegemea mofimu nyingine na huwa na maana kamili.
AINA ZA MOFIMU
Mofimu zinaweza zikagawanywa katika makundi mawili kwa misingi ya kikazi yaani mofimu za kileksika na mofimu zakisarufi. Pia zinaweza kugawanywa katika makundi mawili kwa msingi wa kimuundo na kupata mofimu huru na mofimu tegemezi.
MOFIMU HURU (Mofimu sabili/mofimu za kileksika)
Hizi ni mofimu ambazo husimama zenyewe zinaumbo dogo zaidi bila kupoteza maana. Aina hiyo ya mofimu hujitokeza katika aina mbali mbali za maneno;
Mfano baba, Mama, kaka, na winnie ni nomino
-chafu, bovu, fupi, zuri na tamu ni vivumishi.
-Hata, lakini, kama, mpaka, au- viunganishi
-Arifu, tafiti, samehe- vitenzi
Mofimu zote huru huwa na kazi ya kileksika
MOFIMU TEGEMEZI
Hizi ni mofimu ambazo haziwezi kusimama ili kukamilisha dhana iliyokusudiwa. Mofimu tegemezi hujumuisha mofimu awali, mzizi, na mofimu tamati.Mpangilio wa
mofimu hizo au mfungamano wa mofimu hizo huunda neno. Mofimu hutumika katika kuunda maneno
N.B Mofimu tegemezi zinapofungana huunda neno tegemezi, mfano: a – na – som – a anasoma, nam – pend – a – nampenda
Mofimu huru huunda neno huru mfano, Baba, mama starehe, jaribu n.k Mfungamano wa mofimu huru na mofimu tegemezi hujenga neno changamano. Mfano; mw – ana – nchi
Mw – ana – anga
KUBAINISHA MOFIMU
Kubainisha mofimu ni kuligawa neno katika mofimu zinazolijenga neno na kueleza kazi za kila mofimu ubabaishaji huo wa mofimu hufuata hatua zifuatazo
Kutambua aina ya neno
– Yaani kama neno hilo ni tegemezi au neno changamano, Neno huru huundwa na mofimu huru na neno tegemezi huundwa na mofimu tegemezi na neno changamano huundwa na moja huru na mengine tegemezi
N: B Neno huru huwa halivunjwi vunjwi kwani huundwa na mofimu huru
Kulitenga neno na kulivunja vunja katika mofimu zinazojenga neno hilo yaani hujenga mofimu awali, mzizi na mofimu tamati.
N: B Mofimu awali, mzizi na mofimu tamati hupatikana katika maneno tegemezi na maneno changamano
Kueleza kazi ya kila mofimu
Mfano: Bainisha mofimu katika maneno yafuatayo
Hatukupendi
Hili ni neno tegemezi
1- Mofimu awali kianzishi, nafsi ya kwanza wingi
2 – Mofimu awali rejeshi kwa mtendwa
3 – Mofimu awali rejeshi kwa mtenda
4 – Mofimu mzizi
5 – Mofimu tamati kanushi
6- Asiyekujua
7- Hili ni neno tegemezi
iii.
1. Mofimu awali nafsi ya tatu umoja
2. Mofimu awali kanushi nafsi ya tatu umoja wakati uliopo
3-Mofimu ya urejeshi kwa mtenda
4-Mofimu awali ya urejeshi kwa mtendwa
5-Mofimu mzizi
- Mofimu tamati
- Kikikitangulia
- Hili ni neno tegemezi
- Mofimu awali nafsi ya tatu umoja
- Mofimu awali kanushi ya nafsi ya tatu umoja wakati uliopo
- 3. Mofimu ya urejeshi kwa mtenda.
- Mofimu mzizi
- Mofimu tamati
- Nimejikata
- Hili ni neno tegemezi
ii 1 – Mofimu awali ya nafsi ya kwanza umoja
2 – Mofimu awali inayoonesha hali timilifu
3 – Mofimu awali ya urejeshi wa kujitendea
4 -Mofimu mzizi
5 -Mofimu tamati
Sipendeki
Hili ni neno tegemezi
-Si- pend – ek –i
1 2 3 4
1. – Si – mofimu awali kanushi nafsi ya kwanza umoja wakati uliopo.
- – pend- mofimu mzizi
- -ek- mofimu tamati ya kutendeka
- -i- mofimu tamati ya ukanushi