NAFASI za Kazi DART Tanzania
DART (Dar Rapid Transit) ni mradi wa usafiri wa haraka wa mabasi uliopo jijini Dar es Salaam, Tanzania. Mradi huu ulianzishwa ili kupunguza msongamano wa magari na kuboresha mfumo wa usafirishaji jijini, ambao kwa muda mrefu ulikuwa na changamoto nyingi. DART inatoa huduma kwa kutumia mabasi ya mwendo kasi yanayopita katika njia maalum (BRT – Bus Rapid Transit), na huhudumia maelfu ya wakazi wa jiji kila siku. Huduma hii inalenga kuwa mbadala wa usafiri wa kuaminika, wa haraka na wa gharama nafuu kwa wakazi wa Dar es Salaam.
Kwa sasa, mradi wa DART uko katika awamu mbalimbali za utekelezaji, ambapo awamu ya kwanza (kutoka Kimara hadi Kivukoni) tayari inafanya kazi. Mabasi ya DART yanafanya safari za mara kwa mara, na vituo vya kisasa vimejengwa katika maeneo mbalimbali ili kurahisisha upandaji na ushukaji wa abiria. Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imekuwa ikihakikisha mradi huu unapanuka hadi maeneo mengine ya jiji. DART imekuwa mfano wa mafanikio ya maboresho ya usafiri barani Afrika, na inatarajiwa kubadilisha zaidi maisha ya wakazi kwa kutoa huduma bora za usafiri mijini.
NAFASI za Kazi DART Tanzania
Ili kuweza kusoma nafasi zilizopo na njia ya kutuma maombi tafadhari bonyeza linki hapo chini