TAMISEMI: FORM FIVE SELECTION 2025/2026

_________________________________________________

MATANGAZO YA AJIRA  KILA SIKU BOFYA HAPA

_________________________________________________

NOTES ZA KIDATO CHA 1 HADI 6 BOFYA HAPA

_________________________________________________

MAGROUP MAPYA YA WHATSAAP BOFYA HAPA

_________________________________________________
MATANGO YA AJIRA BOFYA HAPA
JIUNGE NASI TELEGRAM BOFYA HAPA

TAMISEMI: Form Five Selection 2025/2026

Makala hii ina habari zote muhimu kuhusu uchaguzi wa wanafunzi wa kidato cha tano (Form five selection) na vyuo kwa mwaka wa masomo 2025/2026. Wanafunzi wote waliochaguliwa watajiunga na kidato cha tano na vyuo katika mwaka huo wa masomo.

Tangazo la Orodha ya Uchaguzi wa Kidato cha Tano 2025/2026 (Uchaguzi wa TAMISEMI) ni tukio kubwa linalosubiriwa kwa hamu na wahitimu wa shule za sekondari, pamoja na wazazi na walezi kote Tanzania. Tangazo hili ni mwanzo wa hatua mpya katika safari ya kielimu ya wanafunzi, ikionyesha mabadiliko kutoka elimu ya sekondari ya chini kwenda ya juu, na hatimaye kujiandaa kwa elimu ya juu na soko la kazi.

Kupitia mchakato huu, serikali, kupika Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), hufanya upangaji wa wanafunzi waliofaulu Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE), kwa kuzingatia matokeo yao, uchaguzi maalum, na nafasi zilizopo katika shule mbalimbali nchini. Mchakato huu unafuata kanuni za uwazi, usawa, na haki kwa kila mwanafunzi anayekidhi vigezo vya kielimu.

Katika makala hii, wasomaji wataona mwongozo wa kina kuhusu vigezo vilivyotumika katika upangaji wa wanafunzi, hatua za kufuata ili kuangalia majina ya wanafunzi waliochaguliwa, na taratibu zinazofuata baada ya uchaguzi. Lengo ni kuwasaidia wanafunzi na wazazi kupata taarifa sahihi, kwa wakati ufaao, na kupitia vyanzo rasmi.

Nini Maana ya Form Five Selection?

Form Five Selection ni zoezi rasmi la kupanga na kuwachagua wanafunzi waliofaulu Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne (CSEE) kujiunga na kidato cha tano katika shule mbalimbali za serikali nchini Tanzania. Mfumo huu husaidia kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapangiwa shule kwa haki na kwa kuzingatia ufaulu wao, pamoja na nafasi zilizopo.

Jinsi ya Kuangalia Majina ya Waliochaguliwa Kidato cha Tano 2025/2026 (Form Five Selection)

Kupata orodha rasmi ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano, ni muhimu kufuata taratibu zilizowekwa na TAMISEMI kupia mfumo wa kidijitali. Hapa chini ni hatua muhimu za kufuata:

  1. Tembelea Tovuti Rasmi ya TAMISEMI
    Fungua kivinjari chako, kisha nenda kwenye tovuti rasmi ya TAMISEMI kupia anwani: https://selform.tamisemi.go.tz. Hii ndiyo njia salama na ya kuaminika ya kupata majina ya waliochaguliwa.

  2. Chagua Kipengele cha “Form Five Selection”
    Baada ya kufika kwenye tovuti, bonyeza kwenye kiungo kinachosema “Selection Results” au “Form Five Selection 2025” kufungua ukurasa wa matokeo.

  3. Chagua Mkoa, Wilaya na Shule Aliyosoma
    Chagua jina la mkoa na wilaya uliyofanya mtihani wa Kidato cha Nne, kisha tafuta shule yako kwenye orodha iliyotolewa.

  4. Pakua na Angalia Orodha ya Waliochaguliwa
    Baada ya kuchagua shule, orodha ya wanafunzi waliochaguliwa itaonekana, pamoja na shule walizopangiwa. Majina yataonyeshwa kulingana na ufaulu na masuala waliochagua.

  5. Chukua Hatua Muhimu Baada ya Kupata Taarifa
    Mara utakapoona jina lako na shule uliyopangiwa, hakikisha unachukua hatua muhimu kama vile kujiandaa kwa mahitaji ya shule na kufika kwa wakati.

Tazama Form Five Selection Kupitia Mkoa Wako;

ARUSHA

DAR ES SALAAM

 DODOMA

GEITA

IRINGA

KAGERA

KATAVI

KIGOMA

KILIMANJARO

LINDI

MANYARA

 MARA

MBEYA

MOROGORO

MTWARA

MWANZA

NJOMBE

PWANI

RUKWA

RUVUMA

SHINYANGA

SIMIYU

SINGIDA

SONGWE

TABORA

TANGA

Vigezo Vilivyotumika Katika Uchaguzi wa Form Five

TAMISEMI hufuata vigezo maalum katika zoezi hili la uchaguzi. Baadhi ya vigezo muhimu ni:

  • Ufaulu wa mwanafunzi katika masomo husika

  • Mwelekeo wa tahasusi (Combination) aliouchagua

  • Nafasi zilizopo kwenye shule

  • Usawa wa kijinsia

  • Mahitaji maalum ya baadhi ya shule

Kwa mfano, mwanafunzi aliyefaulu vizuri katika masomo ya sayansi anaweza kupangwa katika shule zenye tahasusi za PCB, PCM, CBG n.k.

Orodha ya Tahasusi (Combinations) Zinazotolewa Kidato cha Tano

Zifuatazo ni baadhi ya tahasusi maarufu zinazopatikana kwenye shule za sekondari za kidato cha tano nchini Tanzania:

  • PCM – Physics, Chemistry, Mathematics

  • PCB – Physics, Chemistry, Biology

  • EGM – Economics, Geography, Mathematics

  • HGL – History, Geography, Language

  • CBG – Chemistry, Biology, Geography

  • HKL – History, Kiswahili, Language

Kila tahasusi inaendana na malengo ya mwanafunzi katika taaluma yake ya baadaye, hivyo uchaguzi wa combination ni muhimu sana.

Nini Cha Kufanya Baada ya Kupangiwa Shule

Baada ya kuona jina lako katika orodha ya TAMISEMI Form Five Selection 2025/2026, fanya yafuatayo:

  • Pakua barua ya wito (Joining Instruction) kutoka kwenye tovuti hiyo hiyo ya TAMISEMI

  • Soma kwa makini maelekezo yote yaliyopo kwenye barua

  • Jiandae kwa mahitaji kama sare, ada, vifaa vya shule, na vyeti muhimu

  • Fika shuleni kwa muda uliopangwa kuanza masomo

Maeneo Muhimu Katika Barua ya Wito

Barua ya wito huwa na taarifa muhimu kama:

  • Tarehe ya kuripoti shuleni

  • Mahitaji ya mwanafunzi

  • Maelezo ya ada na michango mingine

  • Maelekezo ya usafiri na mawasiliano ya shule

Ni muhimu sana kuwasiliana na shule husika mapema endapo kuna swali lolote.

Nini cha Kufanya Kama Hukuchaguliwa?

Iwapo jina lako halimo kwenye orodha ya waliochaguliwa, usivunjike moyo. Unaweza kuchukua hatua zifuatazo:

  • Subiri awamu ya pili ya uchaguzi (kama itatolewa)

  • Tuma maombi ya kujiunga na shule binafsi au vyuo vya kati

  • Wasiliana na ofisi ya elimu ya wilaya kwa ushauri zaidi

Kumbuka kuwa elimu haina mwisho, kuna njia nyingi za kufikia ndoto zako hata kama hukupangwa awamu ya kwanza.

MATANGO YA AJIRA BOFYA HAPA
JIUNGE NASI TELEGRAM BOFYA HAPA

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *