Close Menu
Kisiwa24

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    What's Hot

    Fomu za Kujiunga Kidato cha Kwanza 2026 – TAMISEMI Form One Joining Instructions

    January 4, 2026

    RATIBA Mpya ya Treni Za SGR Dar, Morogoro hadi Dodoma 2026

    January 4, 2026

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026
    Kisiwa24Kisiwa24
    • Home
    • Ajira
    • Michezo
    • Makala
    • Elimu
    Kisiwa24
    Home»Ajira»NAFASI 12 za Kazi Mbulu Town Council July 2025
    Ajira

    NAFASI 12 za Kazi Mbulu Town Council July 2025

    Kisiwa24By Kisiwa24July 1, 2025No Comments5 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Reddit Telegram Email
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

    Mkurugenzi wa Mji Mbulu amepata kibali kipya cha ajira kwa ikama ya mwaka 2024/2025 chenye Kumb.Na FA.97/228/01/A/25 cha tarehe 29 Aprili 2025 kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Kufuatia kibali hicho Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Mbulu anakaribisha maombi kwa Watanzania wenye sifa za kujaza nafasi za kazi zifuatazo :-

    NAFASI 12 za Kazi Mbulu Town Council July 2025

    MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II – NAFASI TANO (05)

    MAJUKUMU YA KAZI

    i. Kuorodhesha barua zinazoingia masijala mwenye regista (IncomingCorrespondence Register)
    ii. Kuorodhesha barua zinazotoka nje ya Taasisi (Outgoing CorrespondenceRegister)
    iii. Kusambaza majalada kwa watendaji (Action Officers)
    iv. Kupokea majalada yanayorudi masijala kutoka kwa watendaji
    v. Kurudisha majalada kwenye shubaka/kabati la majalada (Racks/FillingCabinets) au Mahali Pengine yanapohifadhiwa.
    vi. Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani na nje ya Taasisi (File tracking)

    SIFA ZA MWOMBAJI

    Awe na Elimu ya kidato cha Nne (IV) au cha Sita (VI) aliyehitimu mafunzo ya stashahada/Diploma (NTA Level 6) katika fani ya utunzaji wa kumbukumbu kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali, mwenye ujuzi wa Kompyuta.

    NGAZI YA MSHAHARA
    Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali – TGS C

    DEREVA DARAJA LA II NAFASI TANO (05)

    MAJUKUMU YA KAZI

    i. Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kubaini hali ya usalama wa gari,
    ii. Kuwapeleka Watumishi maeneo mbalimbali kwenye safari za kikazi,
    iii. Kufanya matengenezo madogo madogo ya gari,
    iv. Kutunza na kuandika daftari la safari “log book” kwa safari zote,
    v. Kukusanya na kusambaza nyaraka mbalimbali
    vi. Kufanya usafi wa Gari,
    vii. Kufanya kazi nyingine kadri atakavyoelekezwa na Msimamizi wake.

    SIFA ZA MWOMBAJI

    Kuajiriwa wenye cheti cha Kidato cha Nne (Form IV) na Leseni ya Daraja E au C ya uendeshaji magari ambayo wamefanyia kazi kwa muda usiopungua mwaka mmoja (1)
    bila kusababisha ajali pamoja na vyeti vya mafunzo vilivyowapatia sifa ya kupata madaraja husika. Wawe wamehudhuria mafunzo ya msingi ya Uendeshaji magari
    (Basic Driving Course) yanayotolewa na Chuo cha VETA au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali

    NGAZI YA MSHAHARA

    Kwa kuzingatia Ngazi ya Mshahara ni TGS B

    MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II NAFASI MBILI (2)

    MAJUKUMU YA KAZI

    i. Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na za siri
    ii. Kupokea Wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa.
    iii. Kutunza taarifa za kumbukumbuka za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine
    iv. Kutafuta majalada na nyaraka zinazohitajika katika utekelezaji wa majukumu ya kazi
    v. Kupokea majalada na kusambaza kwa Maofisa walio katika Idara/ Kitengo/ sehemu husika
    vi. Kukusanya, kutunza na kuyarejesha majalada na nyaraka sehemu zinazohusika
    vii. Kupanga dondoo na kufanya maandalizi ya vikao mbalimbali
    viii. Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya Ofisi

    SIFA ZA MWOMBAJI

    Mwombaji anatakiwa awe na Elimu ya kidato cha Nne au Sita wenye Stashahada (Diploma) ya Uhazili au Cheti cha NTA level 6 ya Uhazili. Aidha, wawe wamefaulu somo
    la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 100 kwa dakika moja na kupata progamu za kompyuta za Ofisi kama vile; Word Excel, Powerpoint, Internet, E-mail na Publisher kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.

    MSHAHARA

    Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C.

    MASHARTI YA JUMLA

    i. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania wenye umri wa miaka 18 na usiozidi miaka 45.
    ii. Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha kwenye mfumo wa kuombea ajira Ulemavu walionao kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma.
    iii. Waombaji waambatanishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anuani inayotumika, namba za simu zinazopatikana na anuani ya barua pepe (Email Address) pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
    iv. Maombi yote yaambatane na vyeti vya Elimu na taaluma vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya Kidato cha Nne au Kidato cha Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificate – Cheti cha Mtihani wa Kidato cha nne na cha Sita, Computer Certificate, – Vyeti vya Kitaaluma (Proffessional Certificate from Respective Boards).
    v. Wasailiwa watakaowasilisha Testimonials, Provisional Results, Statement of results, hatiza matokeo za kidato cha IV na VI (form V and form VI results slips) HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI.
    vi. Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na vimethibitishwa na Mamlaka husika (TCU, NECTA na NACTVET).
    vii. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
    viii. Waombaji kazi wa kada ya Dereva II wenye leseni Daraja E au C wanapaswa KUAMBATISHA vyeti vya mafunzo ya Udereva vilivyowapatia sifa ya kupata madaraja husika.
    ix. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa Umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na. CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba, 2010.
    x. Waombaji watakaowasilisha taarifa na sifa za kughushi watachukuliwa hatua za kisheria.
    xi. Wasailiwa ambao majina yao yanatofautiana katika nyaraka zao wanapaswa kuwasilisha Hati ya Kiapo cha Kubadili Jina (Deed Poll) iliyosajiliwa na Wizara ya Ardhi.
    xii. Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 14 Julai, 2025

    BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD PDF YA TANGAZO

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleNAFASI Za Kazi Green Bird College
    Next Article Jinsi Ya Kuangalia Deni TRA
    Kisiwa24

    Related Posts

    Ajira

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026
    Ajira

    NAFASI 33 za Kazi Chuo Cha MUST

    January 3, 2026
    Ajira

    NAFASI 10 za Kazi Halmshauri ya Mji Babati

    January 3, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    Demo
    Top Posts

    Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi ya Sheli

    July 2, 202560 Views

    Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania 2026

    December 21, 202545 Views

    Jinsi ya kuangalia Namba ya leseni ya udereva

    March 9, 202538 Views
    Stay In Touch
    • Facebook
    • YouTube
    • TikTok
    • WhatsApp
    • Twitter
    • Instagram
    Latest Reviews

    Subscribe to Updates

    Get the latest tech news from FooBar about tech, design and biz.

    Demo
    Most Popular

    Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi ya Sheli

    July 2, 202560 Views

    Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania 2026

    December 21, 202545 Views

    Jinsi ya kuangalia Namba ya leseni ya udereva

    March 9, 202538 Views
    Our Picks

    Fomu za Kujiunga Kidato cha Kwanza 2026 – TAMISEMI Form One Joining Instructions

    January 4, 2026

    RATIBA Mpya ya Treni Za SGR Dar, Morogoro hadi Dodoma 2026

    January 4, 2026

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    • Home
    • Buy Now
    © 2026 ThemeSphere. Designed by ThemeSphere.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.