Close Menu
Kisiwa24

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    What's Hot

    Fomu za Kujiunga Kidato cha Kwanza 2026 – TAMISEMI Form One Joining Instructions

    January 4, 2026

    RATIBA Mpya ya Treni Za SGR Dar, Morogoro hadi Dodoma 2026

    January 4, 2026

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026
    Kisiwa24Kisiwa24
    • Home
    • Ajira
    • Michezo
    • Makala
    • Elimu
    Kisiwa24
    Home»Ajira»NAFASI 15 za Kazi Njombe District Council June 2025
    Ajira

    NAFASI 15 za Kazi Njombe District Council June 2025

    Kisiwa24By Kisiwa24June 10, 2025No Comments5 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Reddit Telegram Email
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

    Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kupitia Kibali cha Ajira Mpya chenye kumb. Na. FA.97/228/01/A/25 cha tarehe 29 Aprili, 2025 chenye nafasi ya Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja II (4), Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II (5), Dereva Daraja II (8) kutoka kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Hivyo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Njombe anatangaza nafasi za kazi na anakaribisha maombi kwa watanzania wenye sifa za kujaza nafasi hizo kama ifuatavyo:-

    NAFASI za Kazi Njombe District Council June 2025

    MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II NAFASI 2

    MAJUKUMU YA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II

    i. Kuorodhesha barua zinazoingia masijala kwenye regista (incoming correspondence register).
    ii. Kuorodhesha barua zinazotoka nje ya Taasisi (Outgoing Correspondence Register)
    iii. Kusambaza majalada kwa Watendaji (Action Office).
    iv. Kupokea majalada yanayorudi masijala kutoka kwa watendaji.
    v. Kutafuta kumbukumbu/nyaraka au majalada yanayohitajika na watendaji.
    vi. Kurudisha majalada kwenye shubaka/kabati la majalada (Racks/Filling cabinets) au mahali pengine yanapohifadhiwa.
    vii. Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani na nje ya Taasisi (File tracking).

    SIFA ZA MWOMBAJI

    Awe na Elimu ya kidato cha Nne (IV) au cha Sita (VI) aliehitimu mafunzo ya stashahada/Diploma (NTA Level 6) katika fani ya Utunzaji wa Kumbukumbu kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali, wenye ujuzi wa kutumia kompyuta.

    NGAZI YA MSHAHARA

    Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali – TGS C1

    MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II NAFASI 5

    MAJUKUMU YA KAZI YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI II

    i. Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na za siri.
    ii. Kupokea wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa.
    iii. Kutunza taarifa na kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za mkuu wake na ratiba ya kazi zingine.
    iv. Kutafuta majalada na nyaraka zinazohitajika katika utekelezaji wa majukumu ya kazi.
    v. Kupokea majalada na kusambaza kwa maofisa walio katika Idara/kitengo/Sehemu husika.
    vi. Kukusanya, kutunza na kuyarejesha majalada na nyaraka sehemu zinazohusika.
    vii. Kupanga dondoo na kufanya maandalizi ya vikao mbalimbali, na
    viii. Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya ofisi.

    SIFA ZA MWOMBAJI

    Kuajiriwa mwenye elimu ya Kidato cha nne au sita wenye stashahada (Diploma) ya Uhazili au cheti NTA LEVEL 6 ya uhazili. Aidha wawe wamefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingeleza maneno 100 kwa dakika moja na kupata programu za Compyuta za ofisi kama vile Word, Exel, Powerpoint, Windows, Internet, E-mail na Publisher kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.

    NGAZI YA MSHAHARA

    Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali- TGS C1

    DEREVA DARAJA LA Il – NAFASI 8

    MAJUKUMU YA KAZI YA DEREVA DARAJA II

    i. Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kubaini hali ya usalama wa gari.
    ii. Kuwapeleka watumishi maeneo mbalimbali kwenye safari za kikazi.
    iii. Kufanya matengenezo madogomadogo ya gari.
    iv. Kukusanya na kusambaza nyaraka mbalimbali.
    v. Kujaza na kutunza taarifa za safari zote katika daftari la safari (log book)
    vi. Kufanya usafi wa gari.

    SIFA ZA MWOMBAJI

    Kuajiriwa wenye cheti cha Kidato cha Nne (Form IV) na Leseni ya Daraja E au C ya uendeshaji magari ambayo wamefanyia kazi kwa muda usiopungua mwaka mmoja (1) bila kusababisha ajali pamoja na vyeti vya mafunzo vilivyowapatia sifa ya kupata madaraja husika. Wawe wamehudhuria mafunzo ya msingi ya Uendeshaji magari (Basic Driving Course) yanayotolewa na Chuo cha VETA au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.

    NGAZI YA MSHAHARA

    Kwa kuzingatia ngazi ya Mshahara wa Serikali – TGS B1 kwa mwezi

    MASHARTI YA JUMLA YA WAOMBAJI WA NAFASI ZA KAZI

    i. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri wa kuanzia miaka18 na usiozidi miaka 45 isipokuwa kwa wale tu walioko kazini Serikalini;
    ii. Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha kwenye Mfumo wa kuombea ajira ulemavu walionao kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma
    iii. Waombaji wote waambatishe maelezo binafsi yaliyojitosheleza (Detail Curriculum Vitae) yenye anuani inayotumika, namba za simu zinazopatikana na Anuani ya Barua Pepe (E-mail address) pamoja na majina ya wadhamini (Referees) watatu wa kuaminika.
    iv. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detail C.V) yenye anuani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika;
    v. Maombi yote yaambatane na vyeti vya Elimu na Taaluma vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya Kidato cha Nne au Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates, – Cheti cha mtihani wa Kidato cha IV na
    VI, – Computer Certificate, – Vyeti vya Kitaaluma (Professional Certificate from Respective Boards);
    vi. “Testmonial“, ‘‘Provisional Results“, “Statement of results“, hati ya matokeo ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
    vii. Waombaji waliosoma nje ya Nchi wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na vimethibitishwa na Mamlaka husika (TCU, NECTA na NACTE).
    viii. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi.
    ix. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa Umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na. CAC.45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba, 2010.
    x. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
    xi. Wakatakao kidhi Sifa zinazotakiwa ndio pekee watakaoitwa katika Usahili.
    xii. Waombaji kazi wa kada ya Dereva II wenye leseni Daraja E au C wanapaswa KUAMBATISHA vyeti vya mafunzo ya Udereva vilivyowapatia sifa ya kupata madaraja husika
    xiii. Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 24/6/2025

    • BONYEZA HAPA KUPAKUA PDF YA TANGAZO

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleNAFASI za Kazi Morogoro District Council June 2025
    Next Article NAFASI za Kazi Newala District Council June 2025
    Kisiwa24

    Related Posts

    Ajira

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026
    Ajira

    NAFASI 33 za Kazi Chuo Cha MUST

    January 3, 2026
    Ajira

    NAFASI 10 za Kazi Halmshauri ya Mji Babati

    January 3, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    Demo
    Top Posts

    Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi ya Sheli

    July 2, 202560 Views

    Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania 2026

    December 21, 202545 Views

    Jinsi ya kuangalia Namba ya leseni ya udereva

    March 9, 202538 Views
    Stay In Touch
    • Facebook
    • YouTube
    • TikTok
    • WhatsApp
    • Twitter
    • Instagram
    Latest Reviews

    Subscribe to Updates

    Get the latest tech news from FooBar about tech, design and biz.

    Demo
    Most Popular

    Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi ya Sheli

    July 2, 202560 Views

    Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania 2026

    December 21, 202545 Views

    Jinsi ya kuangalia Namba ya leseni ya udereva

    March 9, 202538 Views
    Our Picks

    Fomu za Kujiunga Kidato cha Kwanza 2026 – TAMISEMI Form One Joining Instructions

    January 4, 2026

    RATIBA Mpya ya Treni Za SGR Dar, Morogoro hadi Dodoma 2026

    January 4, 2026

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    • Home
    • Buy Now
    © 2026 ThemeSphere. Designed by ThemeSphere.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.