Close Menu
Kisiwa24

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    What's Hot

    Fomu za Kujiunga Kidato cha Kwanza 2026 – TAMISEMI Form One Joining Instructions

    January 4, 2026

    RATIBA Mpya ya Treni Za SGR Dar, Morogoro hadi Dodoma 2026

    January 4, 2026

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026
    Kisiwa24Kisiwa24
    • Home
    • Ajira
    • Michezo
    • Makala
    • Elimu
    Kisiwa24
    Home»Ajira»Nafasi 8 za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Ngara May 2025
    Ajira

    Nafasi 8 za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Ngara May 2025

    Kisiwa24By Kisiwa24May 30, 2025No Comments4 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Reddit Telegram Email
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

    Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara amepokea kibali kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilichotoa idhini ya utekelezaji wa nafasi za Ajira Mpya katika ikama ya mwaka wa fedha 2024/2025 chenye Kumb. Na. FA. 97/228/01/A/25 cha tarehe 29 Aprili, 2025. Hivyo anapenda kuwatangazia watanzania wote wenye sifa kutuma maombi ya kazi katika nafasi zifuatazo:-

    Nafasi 8 za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Ngara May 2025

    MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II – NAFASI 4

    KAZI NA MAJUMKUMU

    i. Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na siri,
    ii.Kupokea wageni na kuwasilisha shida zao na kuwaelekeza wanapoweza kusaidiwa;
    iii. Kutafuta majalada na nyaraka zinazohitajika katika utekelezaji wa majukumu ya kazi;
    iv. Kupokea majalada na kusambaza kwa maofisa walio katika Divisheni, Vitengo na Sehemu zinazohusika;
    v.Kukusanya, kutunza na kuyarejesha majalada na nyaraka sehemu zinazohusika;
    vi. Kupanga dondoo na kufanya maandalizi ya vikao mbalimbali; na
    vii. Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya ofisi.

    SIFA ZA MUOMBAJI

    Awe na Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV) au cha Sita (Form VI) na amehitimu Stashahada/Diploma ya Uhazili au Cheti cha NTA Level 6 ya Uhazili. Aidha awe amefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 100 kwa Dakika Moja na kupata program za kompyuta za ofisi kama vile:- Word, Excel, Power Point, Internet, Email, na Publisher kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.

    NGAZI YA MSHAHARA

    Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali – TGS C 1

    MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II – NAFASI 04

    KAZI NA MAJUMKUMU

    i. Kuorodhesha barua zinazoingia masijala kwenye Rejista (Incoming Correspondence Register)
    ii. Kuorodhesha barua zinazotoka nje ya taasisi (Outgoing Correspondence Register).
    iii. Kusambaza majalada kwa Watendaji (Action Officers).
    iv. Kupokea Majalada kutoka kwa Watendaji (Action Officers).
    v. Kupokea majalada yanayorudi kutoka kwa Watendaji.
    vi. Kurudisha masijala kwenye Shabaka/ Kabati la Masijala (Racks/Filling Cabinets) au mahala pengine yanapohifadhiwa.
    vii. Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani ya Taasisi (File Tracking).

    SIFA ZA MUOMBAJI

    Awe na Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV) au cha Sita (Form VI). Awe na cheti cha Stashahada (Diploma) (NTA LEVEL 6) cha utunzaji wa kumbukumbu katika fani ya Utunzaji wa Kumbukumbu
    kutoka vyuo vinavyotambuliwa na serikali, na mwenye ujuzi wa Kompyuta.

    NGAZI YA MSHAHARA

    Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali TGS C 1

    MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI

    i. Waombaji wote wawe ni raia wa Tanzania wenye umri usiozidi miaka 45 na umri usiopungua miaka 18,
    ii. Waombaji waambatanishe Cheti cha Kuzaliwa,
    iii. Waombaji waambatanishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye Anuani, Namba za Simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (Referees) wa kuaminika,
    iv. Waombaji wote waweke nakala za vyeti vya taaluma na vyeti vya Kidato cha Nne na Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika kwenye Ajira Portal, Testimonials “Provision Results”, “Statement of Results” Hati ya Matokeo ya Kidato cha Nne na Sita HAVIKUBALIKI,
    v. Waombaji wote waweke picha mbili “Passport Size” ya hivi karibuni katika ukurasa wa Ajira Portal,
    vi. Waombaji waliosoma nje ya nchi wahakikishe vyeti vyao vinahakikiwa na kuthibitishwa na mamlaka husika yaani TCU, NECTA na NACTE,
    vii. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi,
    viii. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katikan Utumishi wa Umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka wenye Kumb. Na. CAC.45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba, 2010,
    ix. Uwasilishwaji taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria,
    x. Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 12 Juni, 2025, MUHIMU: Kumbuka kuambatisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwa pamoja na vyeti vya elimu na anuani.

    • BONYEZA HAPA KUPAKUA TANGAZO LOTE

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleNafasi 15 za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Biharamulo May 2025
    Next Article Majina ya Walioitwa Kazini Halmashauri Ya Manispaa Ya Kinondoni Na Temeke 30 Mei 2025
    Kisiwa24

    Related Posts

    Ajira

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026
    Ajira

    NAFASI 33 za Kazi Chuo Cha MUST

    January 3, 2026
    Ajira

    NAFASI 10 za Kazi Halmshauri ya Mji Babati

    January 3, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    Demo
    Top Posts

    Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi ya Sheli

    July 2, 202567 Views

    Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania 2026

    December 21, 202545 Views

    Jinsi ya kuangalia Namba ya leseni ya udereva

    March 9, 202538 Views
    Stay In Touch
    • Facebook
    • YouTube
    • TikTok
    • WhatsApp
    • Twitter
    • Instagram
    Latest Reviews

    Subscribe to Updates

    Get the latest tech news from FooBar about tech, design and biz.

    Demo
    Most Popular

    Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi ya Sheli

    July 2, 202567 Views

    Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania 2026

    December 21, 202545 Views

    Jinsi ya kuangalia Namba ya leseni ya udereva

    March 9, 202538 Views
    Our Picks

    Fomu za Kujiunga Kidato cha Kwanza 2026 – TAMISEMI Form One Joining Instructions

    January 4, 2026

    RATIBA Mpya ya Treni Za SGR Dar, Morogoro hadi Dodoma 2026

    January 4, 2026

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    • Home
    • Buy Now
    © 2026 ThemeSphere. Designed by ThemeSphere.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.