Close Menu
Kisiwa24

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    What's Hot

    Fomu za Kujiunga Kidato cha Kwanza 2026 – TAMISEMI Form One Joining Instructions

    January 4, 2026

    RATIBA Mpya ya Treni Za SGR Dar, Morogoro hadi Dodoma 2026

    January 4, 2026

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026
    Kisiwa24Kisiwa24
    • Home
    • Ajira
    • Michezo
    • Makala
    • Elimu
    Kisiwa24
    Home»Ajira»Nafasi Mpya Za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Nzega Augost 2024
    Ajira

    Nafasi Mpya Za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Nzega Augost 2024

    Kisiwa24By Kisiwa24August 4, 2024No Comments5 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Reddit Telegram Email
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

    Nafasi Mpya Za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Nzega Augost 2024

    Habari hii na nyingine nyingi zinapatikana kwenye telegram channel yetu na WhatsApp channel yetu tumia linki hapo chini kujiunga

    BONYEZA HAPA KUJIUNGA NA TELEGRAM CHANNEL YETU
    BONYEZA HAPA KUJIUNGA NA WHATSAPP CHANNEL YETU

    Mkurugenzi amepata kibali kipya cha ajira kwa ikama ya mwaka 2023/2024chenye Kumb. Na. FA. 97/288/01/09 cha tarehe 25.06.2024 kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Kufuatia kibali hicho Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Nzega anakaribisha maombi kwa watanzania wenye sifa za kujaza nafasi za kazi zifuatazo :-

     

    MTENDAJI WA KIJIJI III – NAFASI (12)
    MAJUKUMU YA KAZI
    i. Mtendaji Mkuu wa Serikali ya kijiji;

    ii. Katibu wa Kamati ya kijiji;

    iii. Mratibu wa utekelezaji wa Sera na Sheria zinazotekelezwa na
    Halmashauri katika Kijiji;

    iv. Mshauri wa Kamati ya Kijiji kuhusu Mipango ya Maendeleo katika Kijiji;

    v. Msimamizi wa Utekelezaji wa Sheria ndogo pamoja na Sheria nyingine zinazotumika katika Kijiji;

    vi. Msimamizi wa Mtekelezaji wa mikakati mbalimbali inayohusu uondoaji wa njaa na Umasikini katika Kijiji;

    vii. Msimamizi wa Mtekelezaji wa mikakati mbalimbali inayohusu uondoaji wa njaa na Umasikini katika Kijiji;

    viii. Kusimamia Ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri na kutunza kumbukumbu za walipa kodi; na

    ix. Atawajibika kwa Mtendaji wa Kata.

    SIFA ZA MWOMBAJI
    Awe amehitimu Elimu ya Kidato cha Nne (IV) au Kidato cha Sita (VI), awe amehitimu mafunzo ya Astashahada katika moja ya fani zifuatazo; Sheria, Elimu ya Jamii, Usimamizi wa Fedha, Maendeleo ya Jamii na Sayansi ya sanaa kutoka chuo cha Serikali za Mitaa au Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.

    NGAZI YA MSHAHARA
    Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali – TGS B.

    MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II – NAFASI (03)

    MAJUKUMU YA KAZI
    i. Kuorodhesha barua zinazoingia masijala mwenye regista (Incoming Correspondence Register)

    ii. Kuorodhesha barua zinazotoka nje ya Taasisi (Outgoing CorrespondenceRegister)

    iii. Kusambaza majalada kwa watendaji (Action Officers)

    iv. Kupokea majalada yanayorudi masijala kutoka kwa watendaji

    v. Kutafuta kumbukumbu/Nyaraka au majalada yanayohitajika na watendaji

    vi. Kurudisha majalada kwenye shubaka/kabati la majalada (Racks/FillingCabinets) au Mahali Pengine yanapohifadhiwa.

    vii. Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani na nje ya Taasisi (File tracking)

    SIFA ZA MWOMBAJI
    Awe na Elimu ya kidato cha Nne (IV) au cha Sita (VI) aliyehitimu mafunzo ya stashahada/Diploma (NTA Level 6) katika fani ya utunzaji wa kumbukumbu kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali, wenye ujuzi wa kutumia kompyuta

    NGAZI YA MSHAHARA
    Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali – TGS C

    MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II (3)

    MAJUKUMU YA KAZI

    i. Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na za siri

    ii. Kupokea Wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa.

    iii. Kutunza taarifa za kumbukumbuka za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine

    iv. Kutafuta majalada na nyaraka zinazohitajika katika utekelezaji wa majukumu ya kazi

    v. Kupokea majalada na kusambaza kwa Maofisa walio katika Idara/ Kitengo/ sehemu husika

    vi. Kukusanya, kutunza na kuyarejesha majalada na nyaraka sehemu zinazohusika

    vii. Kupanga dondoo na kufanya maandalizi ya vikao mbalimbali

    viii. Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya Ofisi

    ix. Kufanya kazi nyingine atakavyoelekezwa na Msimamizi wake.

    SIFA ZA MWOMBAJI
    Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha Nne (Form IV) au cha Sita (Form VI), wenye stashahada (Diploma) ya Uhazili au cheti cha (NTA Level 6) yauhazili. Aidha wawe wamefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kingereza maneno 100 kwa dakika moja na kupata program za kompyuta za ofisi kama vile; Word, Excel, PowerPoint, Internet, E-mail na Publisher kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.

    MSHAHARA
    Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C.

    MASHARTI YA JUMLA
    i. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania wenye umri wa miaka 18 na usiozidi miaka 45 isipokuwa kwa wale tu walioko kazini – Serikalini.

    ii. Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha kwenye mfumo wa kuombea ajira aina ya Ulemavu walionao kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

    iii. Waombaji waambatanishe maelezo binafsi yaliyojitosheleza Curriculum Vitae (CV) yenye Anuani inayotumika, namba za simu zinazopatikana na Anuani ya barua pepe (E-mail adress) pamoja na majina ya wadhamini (Referees) watatu wa kuaminika.

    “Provisional “/Testimonials”/ “Statement of results” na hati za matokeo za kidato cha Nne na Sita (Form IV and Form VI results slip)HAVITAKUBALIWA.

    iv. Waombaji wote waambatanishe cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na Mwanasheria/Wakili.

    v. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.

    vi. Waombaji ambao tayari ni Watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingia katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazi kwa waajiri wao na waajiri wao wajiridhishe ipasavyo.

    vii. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa Umma, wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na. CAC.45/257/01/D/140 wa tarehe 30
    Novemba, 2010.

    viii. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya Kidato cha Nne, kidato cha Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo
    mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.

    ix. Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Dilpoma/Certificates, – Cheti cha mtihani wa Kidato cha IV na VI, – Computer Certificate, – Vyeti vya Kitaaluma (Professional Certificate from Respective Boards).

    x. Waombaji waliosoma nje ya Nchi wahakikishe vyeti vyao vimethibitishwa na Mamlaka husika (TCU, NECTA au NACTVET).

    xi. Uwasilishaji wa Taarifa na Sifa za kughushi, wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.

    xii. Barua ya maombi iandikwe kwa Kiswahili au Kiingereza.

    xiii. Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 14 Agosti, 2024.

    xiv. MUHIMU: Kumbuka kuambatanisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwa pamoja na vyeti vya elimu, aidha anuani ya barua hiyo ielekezwe kwa:

    Mkurugenzi Mtendaji,
    Halmashauri ya Wilaya ya Nzega,
    S.L.P 4,
    NZEGA-TABORA

    xv. Maombi yote ya kazi yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo; https://portal.ajira.go.tz (Anuani hii pia inapatikana kwenye Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa “Recruitment Portal”

    xvi. Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu ulioainishwa katika
    tangazo hili HAYATAFIKIRIWA

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleHabari kubwa Katika Magazeti ya leo Jumatano Julai 31 2024
    Next Article Nafasi Mpya Za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro August 2024
    Kisiwa24

    Related Posts

    Ajira

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026
    Ajira

    NAFASI 33 za Kazi Chuo Cha MUST

    January 3, 2026
    Ajira

    NAFASI 10 za Kazi Halmshauri ya Mji Babati

    January 3, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    Demo
    Top Posts

    Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi ya Sheli

    July 2, 202560 Views

    Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania 2026

    December 21, 202537 Views

    Jinsi ya kuangalia Namba ya leseni ya udereva

    March 9, 202537 Views
    Stay In Touch
    • Facebook
    • YouTube
    • TikTok
    • WhatsApp
    • Twitter
    • Instagram
    Latest Reviews

    Subscribe to Updates

    Get the latest tech news from FooBar about tech, design and biz.

    Demo
    Most Popular

    Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi ya Sheli

    July 2, 202560 Views

    Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania 2026

    December 21, 202537 Views

    Jinsi ya kuangalia Namba ya leseni ya udereva

    March 9, 202537 Views
    Our Picks

    Fomu za Kujiunga Kidato cha Kwanza 2026 – TAMISEMI Form One Joining Instructions

    January 4, 2026

    RATIBA Mpya ya Treni Za SGR Dar, Morogoro hadi Dodoma 2026

    January 4, 2026

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    • Home
    • Buy Now
    © 2026 ThemeSphere. Designed by ThemeSphere.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.