Close Menu
Kisiwa24

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    What's Hot

    Fomu za Kujiunga Kidato cha Kwanza 2026 – TAMISEMI Form One Joining Instructions

    January 4, 2026

    RATIBA Mpya ya Treni Za SGR Dar, Morogoro hadi Dodoma 2026

    January 4, 2026

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026
    Kisiwa24Kisiwa24
    • Home
    • Ajira
    • Michezo
    • Makala
    • Elimu
    Kisiwa24
    Home»Ajira»Nafasi Mpya 25 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe
    Ajira

    Nafasi Mpya 25 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe

    Kisiwa24By Kisiwa24July 24, 2024No Comments5 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Reddit Telegram Email
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

    Nafasi Mpya 25 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe

    Habari hii na nyingine nyingi zinapatikana kwenye telegram channel yetu na WhatsApp channel yetu tumia linki hapo chini kujiunga

    BONYEZA HAPA KUJIUNGA NA TELEGRAM CHANNEL YETU
    BONYEZA HAPA KUJIUNGA NA WHATSAPP CHANNEL YETU

     

    Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe amepokea kibali cha ajira mpya kutoka kwa katibu mkuu OR – Utumishi chenye Kumbu. Na. FA. 97/288/01/09 cha tarehe 25.06.2024. Hivyo anapenda kuwatangazia watanzania wote wenye sifa kutuma maombi kwa kada tatu (03) kama zilivyoanishwa kwa kuzingatia sifa tajwa:-

    Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Yatangaza Nafasi za Kazi (Mwisho 25/07/2024)

    Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja La II (“Office Management Secretary II”) Nafasi 5.

    Sifa Za Mwombaji.

    kuajiriwa wa wahitimu wa kidato cha nne au sita wenye stashahada (Diploma) ya Uhazili au Cheti cha NTA level 6 ya uhazili. aidha, wawe wamefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 100 kwa dakika moja na kupata program za kompyuta za ofisi kama vile Word, Excel, Powerpoint, Internet, E-mail na Publisher kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na serikali.

    Kazi Na Majukumu Ya Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja La II.

    1. Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na za siri.
    2. Kupokea wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa.
    3. Kutunza taarifa na kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za mkuu wake na ratiba za kazi zingine.
    4. Kutafuta majalada na nyaraka zinazohitajika katika utekelezaji wa majukumu ya kazi.
    5. Kupokea majalada na kusambaza kwa maofisa walio katika idara/kitengo/sehemu husika.
    6. Kukusanya, kutunza na kuyarejesha majalada na nyaraka sehemu zinazohusika.
    7. Kupanga dondoo na kufanya maandalizi ya vikao mbalimbali na
    8. Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya ofisi.

    Msaidizi Wa Kumbukumbu II (“Records Management Assistant II”) Nafasi 5

    Sifa Za Mwombaji.

    Awe na Elimu ya Kidato cha Nne (FORM IV) au cha Sita (FORM VI) aliyehitimu mafunzo ya Stashahada/Diploma (NTA level 6) katika fani ya Masijala kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali, wenye ujuzi wa kompyuta.

    1. Kazi Na Majukumu Ya Msaidizi Wa Kumbukumbu II.
    2. Kuorodhesha barua zinazoingia masijala kwenye rejista (incoming Correspondence register)
    3. Kuorodhesha barua zinazotoka nje ya taasisi kwenye rejista (outgoing correspondence register)
    4. Kusambaza majalada kwa watendaji (action officers)
    5. Kupokea majalada yanayorudi masjala toka kwa watendaji.
    6. Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/majalada yanayohitajika na watendaji:
    7. Kurudisha majalada kwenye kabati la majalada (racks/filling cabinets) au mahali pengine yanapohifadhiwa.
    8. Kufuatilia mzunguko wa majalada ndani ya Taasisi (file tracking)
    9. Kutekeleza kazi zozote atakazokuwa amepangiwa na msimamizi wake wa kazi.

     

    Mtendaji Wa Kijiji Daraja La Iii – Nafasi 15.

    Sifa Za Mwombaji.

    Kuajiriwa mwenye Elimu ya Kidato cha Nne au Sita aliyehitimu mafunzo ya Astashahada/Cheti (NTA Level 5) katika mojawapo ya fani zifuatazo:

    • Utawala, Sheria
    • Elimu ya Jamii, Usimamizi wa Fedha, Maendeleo ya Jamii na Sayansi ya Sanaa kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.

    Kazi Na Majukumu Ya Mtendaji Wa Kijiji.

    1. Kuwa Afisa Masuli na Mtendaji Mkuu wa Serikali ya Kijiji.
    2. Kusimamia ulinzi na usalama wa raia na mali zao, kuwa mlinzi wa amani na msimamizi wa utawala bora katika kijiji.
    3. Kuratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya kijiji.
    4. Kuwa Katibu wa mikutano na kamati zote za Halmashauri ya Kijiji.
    5. Kutafsiri na kusimamia sera, sheria na taratibu:
    6. Kuandaa taarifa za utekelezaji wa kazi katika eneo la kazi na kuhamasisha wananchi katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kuondoa njaa, umaskini na kuongeza uzalishaji mali.
    7. Kuwa kiongozi wa wakuu wa vitengo vya kitaalam katika kijiji:
    8. Kusimamia, kukusanya na kuhifadhi kumbukumbu zote na nyaraka za kijiji
    9. Kuwa mwenyekiti wa kikao cha wataalamu katika kijiji
    10. Kusimamia utungaji wa sheria ndogo za kijiji.
    11. Kupokea, kusikiliza na kutatua malalamiko na migogoro ya wananchi na;
    12. Atawajibika kwa mtendaji wa kata.

    Masharti Ya Ujumla Kwa Waombaji

    1. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania wenye umri wa miaka 18 na usiozidi miaka 45 isipokuwa kwa wale tu walioko kazini Serikalini.
    2. Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha kwenye mfumo wa kuombea ajira aina ya Ulemavu walionao kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.
    3. Waombaji waambatanishe maelezo binafsi yaliyojitosheleza Carriculum Vitae (CV) yenye Anuani inayotumika, namba za simu zinazopatikana na Anuani ya barua pepe (E-mail adress) pamoja na majina ya wadhamini (Referees) watatu wa kuaminika.
    4. “Provisional “/Testimonials”/ “Statement of results” na hati za matokeo za kidato cha Nne na Sita (Form IV and Form VI results slip) HAVITAKUBALIWA.
    5. Waombaji wote waambatanishe cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na Mwanasheria/Wakili.
    6. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
    7. Waombaji ambao tayari ni Watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingia katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazi kwa waajiri wao na waajiri wao wajiridhishe ipasavyo.
    8. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa Umma, wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na. CAC.45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba, 2010.
    9. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya Kidato cha Nne, kidato cha Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Dilpoma/Certificates, – Cheti cha mtihani wa Kidato cha IV na VI, – Computer Certificate, – Vyeti vya Kitaaluma (Professional Certificate from Respective Boards).
    10. Waombaji walisoma nje ya Nchi wahakikishe vyeti vyao vimethibitishwa na Mamlaka husika (TCU, NECTA na NACTE).
    11. Uwasilishaji wa Taarifa na Sifa za kughushi, wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
    12. Barua ya maombi iandikwe kwa Kiswahili au Kiingereza.

    Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 25 Julai, 2024

    Kumbuka kuambatanisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwa pamoja na vyeti vya elimu, aidha anuani ya barua hiyo ielekezwe kwa:

    • Mkurugenzi Mtendaji (W),
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe,
    • 28 Barabara ya Bomani,
    • S.L.P 28001,
    • 61401 Kisarawe,
    • KISARAWE.

    Jinsi Ya Kutuma Maombi

    Maombi yote ya kazi yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo; https://portal.ajira.go.tz (Anuani hii pia inapatikana kwenye Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa “Recruitment Portal”

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleHabari kubwa Katika Magazeti ya leo Jumatano ya July 24, 2024
    Next Article Nafasi Mpya 29 za Kazi Halmashauri Ya Wilaya Ya Mbogwe
    Kisiwa24

    Related Posts

    Ajira

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026
    Ajira

    NAFASI 33 za Kazi Chuo Cha MUST

    January 3, 2026
    Ajira

    NAFASI 10 za Kazi Halmshauri ya Mji Babati

    January 3, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    Demo
    Top Posts

    Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi ya Sheli

    July 2, 202560 Views

    Jinsi ya kuangalia Namba ya leseni ya udereva

    March 9, 202537 Views

    Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania 2026

    December 21, 202536 Views
    Stay In Touch
    • Facebook
    • YouTube
    • TikTok
    • WhatsApp
    • Twitter
    • Instagram
    Latest Reviews

    Subscribe to Updates

    Get the latest tech news from FooBar about tech, design and biz.

    Demo
    Most Popular

    Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi ya Sheli

    July 2, 202560 Views

    Jinsi ya kuangalia Namba ya leseni ya udereva

    March 9, 202537 Views

    Link Za Magroup Ya WhatsApp Tanzania 2026

    December 21, 202536 Views
    Our Picks

    Fomu za Kujiunga Kidato cha Kwanza 2026 – TAMISEMI Form One Joining Instructions

    January 4, 2026

    RATIBA Mpya ya Treni Za SGR Dar, Morogoro hadi Dodoma 2026

    January 4, 2026

    NAFASI 07 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Gairo

    January 3, 2026

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    • Home
    • Buy Now
    © 2026 ThemeSphere. Designed by ThemeSphere.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.